2013 KCSE Kiswahili Past Paper-Free KCSE Past Papers with Answers.

2013 KCSE Kiswahili Past Paper

KCSE Past Papers Kiswahili 2013

4.2.1 Kiswahili Paper 1 (102/1)

1.Lazima:

Wewe ni meneja katika kampuni ya Jitihada ambapo pamekuwa na visa vya ukiukaji wa maadili ya kikazi. Waandikie wafanyakazi memo kuwaonya dhidi ya jambo hili.

2 .“Rununu (simutamba) imeleta alhari mbaya katika jamii.“ Jadili.

3 Andika kisa kitakachodhihirisha maana ya methaliz Usitukane wakunga na uzazi ungalipo

4 Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo:

Moyo wangu ulidunda kwa matarajio makuu

4.2.2 Kiswahili Paper 2 (102/2)

UFAHAMU: (Alama 15)

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali. Gari lake kuukuu lilikuwa linapambana na barabara yenye mashimo yaliyoshiba na kutapika maji ya mvua ambayo sasa ilikuwa inaanza kupusa.

Japo daima alipambana na usukani kunako mashimo haya yaliyotosha kuitwa magenge, alishukuru kwa hali hii.

Vipi angeweza kulidhibiti gari lake hili kwenye barabara iliyosakafiwa nayo ikahitimu? Magurudumu haya yaliyong’ara kama upara wa shaibu aliyekula chumvi hadi ikamwogopa yangetii uelekezi wake?

Mara ngapi gari hili limetaka kumwasi barabarani?

Haya yalikuwa baadhi ya maswali yaliyompitikia akilini.

Hakujitakilifu kutaka kuyapa mji maana mara ile mawazo yake yalitekwa na kubwagwa katika nchi ya mbali – nchi ambayo sasa aliiona kama sinema akilini mwake.

Alipofika nyumbani aliliegesha gari lake na kufululiza ndani.

Siku mbili zilikuwa zimepita akiwa pale kazini.

Madaktari kama yeye hawakuwa wengi.

Alikuwa miongoni mwa madaktari wenye ujuzi katika hospitali hii ya kitaifa.

Wenzake wengi walikuwa wamehamia ughaibuni walikokwenda kutafuta maisha.

Mshahara wao wa mkia wa mbuzi uliwasukuma na kuwatema nje ya nchi yao.

Wengi wa waliohamia ng’ambo waliona vigumu kubaki katika ajira ambayo kivuno chake kilishindwa kumvusha mtu hata nusu ya kwanza ya mwezi.

Malalamishi ya kulilia ujira wa heshima yaligonga kwenye masikio yaliyotiwa zege.

Na kweli wanavyosema, mwenye macho haambiwi tazama.

Basi walitazama hapa na pale wakaona penye mianya ya matumaini, nao wakaiandama.

Hadi leo hii hamna la mno lililofanyika.

Ndiyo maana Daktari Tabibu anarudi nyumbani tangu kuingia kazini hiyo juzi alfajixi.

Hafanyi kwa kuwa katosheka, maana pia yeyc ana dukuduku.

Ana shaka ya mustakabali wake ikiwa mazingira ni haya ya kumsoza, maana umri nao unazidi kumla.

Japo anatia na kutoa, mizani ya hcsabu yake imeasi ulinganifu. Daktari Tabibu waama ni mfungwa. Ametekwa na kuzuiwa katika kupenda na kuchukia mambo.

Ni kama mti uliodumaa.

Anatamani barabara nzuri za lami.

Anatamani mshahara wa kumwezesha kukidhi mahitaji yake na kutimiza majukumu yake ya kimsingi.

Jana amesema na rafiki yake aliye ng’ambo kwa simu ambayo sasa imetulia mkabala naye.

Ingawa mwenzake huyu alikuwa mchangamfu na kumdokolea hali ya maisha ya kuridhisha kule ugenini kama vile wanataaluma kuenziwa, yapo vilevile yaliyomtia unyonge moyoni.

Upweke ndio uliomtia fukuto kuu.

Licha ya hela zote hizo za kupigiwa mfano, watu hawana muda wa kutembeleana na kujuliana hali au hata kukutana tu mkahawani wakashiriki mlo.

Eti ni kila mtu na hamsini zake. Halafu ipo changamoto ya hali ya hewa.

Baridi ya ng‘amb0 haifanyi mzaha katika kumtafuna mtu.

Ni hali tofauti na ile aliyoizoea.

Daktari Tabibu alizitia kauli za rafiki yake kwenye mizani ya moyo wake.

Akawaza ikiwa kweli si bora kulemazwa na mzizimo ugenini badala ya kuishi katika kinamasi cha kuumbuliwa nyumbani.

Kisha punde lilimjia wazo la marehemu nyanyake na wengine kama yeye waliofadhili masomo yake kupilia kwa serikali na njia ya kodi.

Je, si usaliti huu? Vipi aikimbie nchi kabla ya kuihudumia ilhali imemjenga hadi kuwa daktari?

Na je, wafanyakazi wake wa nyumbani watakwenda wapi?Atawaambiaje kuwa sasa hahitaji huduma zao kwa kuwa anakimbia nchi yaks?

Mawazo yake yalikatizwa na simu iliyolia na kumshtua.

Alipoitazama aliiona imeng’ara kwa mwangaza ulioweka wazi jina la mpigaji.

Alifahamu kuwa leo hii tena dharura nyingine ilikuwa inamwalika hospitalini.

Mwili wake ulimsaliti ingawa moyo wake ulimkumbusha kuwa lisilo budi hulendwa.

Hapo ndipo alipoiinua ile simu layari kusema na mwenzake upande wa pili.

“Haloo!” Sauti nyororo kutoka upande wa pili iliita.

“Haloo!”

“Naam! Dharura nyingine lena daklari. Unaombwa kuokoa maisha mengine tena!”

“Haya. Ila mwanzo nitahilaji kujimwagia maji”, na pale pale akaikata ile simu.

Dakmri Tabibu aliingia hamamuni huku kajifunga taulo kiunoni tayari kuoga.A1iyafungulia maji

lakini ule mfereji uligoma kutapika maji. Ulikuwa umekauka kabisa. Daktali Tabibu aliduwaa pale. Aliufunga ule mfereji kabla ya kuiaga bafu.

(a) Eleza sababu nne zinazowafanya walaalamu kuhamia nchi za nje. (alama 4)

(b) “Hakuna masika yasiyokuwa na mbu.” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hali ya waliohamia ng’amb0. (alama 3)

(c) Fafanua athari tatu zinazoikumba nchi ya msimulizi kutokana na uhamiaji ng’ambo wa wataalamu. (alama 3)

(d) Eleza mchango wa teknolojia kwa kurejelea kifungu. (alama 3)

(e) Eleza maana za msamiati ufualao kulingana na taarifa. (alama 2)

(i) kuyapa mji (ii) fukuto UFUPISHO: (Alama 15)

Soma kifungu kifimtacho kisha ujibu maswali.

Wakenya walipoipifisha katiba mpya waliidhinisha mfumo wa ugatuzi.

Katika mfumo huu, mamlaka ya serikali kuu katika uongozi, usimamizi na utumiaji wa rasilimali za nchi hupunguzwa.

Kiasi fulani cha mamlaka hutwaliwa na maeneo ya ugatuzi.

Suala hili halikuzingatiwa katika katiba ya awali ambapo mamlaka yote yalikuwa mikononi mwa serikali kuu.

Kutokana na upana na wingi wa maeneo nchini, iliiwia vigumu serikali kuu kuhakikisha kwamba kulikuwa na usawa wa kimaendeleo katika sehemu zote nchini.

Kwa mujibu wa katiba mpya, scrikali kuu haina budi kuyasaidia maeneo yote ya ugatuzi ili yaweze kujinyanyua kiuchumi na kuboresha hali za maisha za wakazi wake.

Vilevile ni jukumu la kila eneo la ugatuzi kuweka mikakati madhubuti ili kuchunguza na kubainisha rasilimali zote katika maeneo husika.

Hili litasaidia kuvumbua rasilimali ambazo zinaweza kuchangia katika ustawishaji wa maeneo haya.

Maeneo haya pia yanatakiwa kutafuta mbinu zitakazofanikisha uzalishaji na utumiaji wa rasilimali hizi kwa njia endelevu.

Mojawapo ya mbinu hizi ni uongezaji thamani katika rasilimali yoyote inayozalishwa kwenye eneo mahususi.

Maeneo mengi ya ugatuzi nchini humu yanategemea kilimo cha ufugaji kama mhimili wa uchumi.

Licha ya kuwa nguzo, kilimo hiki hakijawahi kupigiwa darubini vizuri kwa lengo la kukiimarisha ili kiwanufaishe wenyeji kikamilifu.

Aghalabu wafugaji wengi huandama mbinu zajadi za ufugaji ambazo haziwahakikishii ongezcko la mapato.

Isitoshe, wafugaji hawa wanakabiliwa na tatizo katika soko la mifugo ambapo wengi hupunjwa na matapeli.

Pamoja na haya, baadhi ya wakazi huuza mifugo nje ya nchi wakiwa wazimawazima bila kuwazia matokeo ya kitendo hiki.<

Si ajabu kuwaona ng’ombc, ngamia, mbuzi na kondoo wakipakiwa kwenye malori na kusafirishwa nje ya nchi.

Ukweli ni kwamba jambo hili ni hatari sana, si kwa uchumi wa maeneo husika tu, bali pia kwa Kenya kwa jumla.

Hii ni kwa kuwa walionunua mifugo wazimawazima wanaweza kuhiari kutowachinja na badala yakc kuwatumia kama mbegu za kuzalisha mifugo wao.

Hapa pana hatari ya rnaeneo haya kupoteza wateja kwani baada ya muda huenda wanaonunua mifugo wakajitosheleza na kukosa kuja kununua mifugo wengine.

hali ikiwa hivyo, maeneo yaliyotegemea soko hili huenda yakalipoteza taratibu, na bila shaka kupoteza natija inayotokana na soko lenyewe.

Ili kudhibiti hali hii, itakuwa bora ikiwa viwanda vya kuchinjia mifugo na kupakia nyama vitajengwa katika maeneo haya ya ugatuzi.

Hili litawawezesha wakazi kuuza nyama badala ya kuuza mifugo wazimawazima.

Fauka ya haya, maeneo haya yatajikinga dhidi ya kupoteza bidhaa zinazotokana na mifugo.

Hizi ni kama vile ngozi, kwato na pembe ambazo bila shaka zina natija kuu.

Ngozi kwa mfano, ni bidhaa muhimu sana katika sekta ya utengenezaji wa mavazi na mifuko.

Viwanda vinavyotumia ngozi kama malighafi vikijengwa katika maeneo haya, wakazi wake watanufaika si haba.

Mathalani, viwanda vya kutengenezea viatu, mishipi, mifuko na nguo vikianzishwa, wawekezaji watalazimika kuanzisha viwanda vingine vitegemezi.

Kadhalika, ni dhahiri kwamba bidhaa zinazotokana na ngozi huhitaji kutiwa nakshi.

Kuanzishwa kwa viwanda hivi basi kutazua haja ya kuanzishwa kwa viwanda vya kutengenezea rangi, pamoja na maduka ya kuuza bidhaa yenyewe.

Isitoshe, gundi ya kugandisha bidhaa hizi itahitajika, hivyo kusababisha haja ya kuanzishwa kwa kiwanda cha gundi.

Matokeo ya shughuli hizi zote ni kuzalishwa kwa nafasi anuwai za kazi kwa wakazi.

Hili litakuwa na matokeo zaidi chanya, hususan kwa vijana.

Badala ya kushiriki ulevi na burudani zinazowahatarisha, wataweza kujitafutia riziki katika viwanda hivi.

Juu ya hayo, mfumo wa ugatuzi utayawczesha maeneo husika kuongezea thamani utoaji wa huduma za kijamii na kiutawala kulingana na mahitaji ya maeneo haya.

Ni muhimu hata hivyo kuzingatia kwamba kila cneo la ugatuzi lina upekee wake, navyo vipaumbele hutofautiana kulingana na maeneo.

Kuna yale ambayo yatasisitiza usalama, mengine ujenzi na uimarishaji wa miundomsingi kama vile barabara, vituo vya afya na hata taasisi za elimu.

La muhimu ni wakazi wa maeneo husika kubainisha ni lipi litatekelezwa kwanza.

Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.

Kufanikiwa kwa mfumo wa ugatuzi kutategemea juhudi za kila mkazi wa eneo husika.

Ni muhimu kila mkazi kujiona kuwa mmiliki wa eneo zima la ugatuzi na kuwajibika katika kuliendeleza kwa hali na mali.

Uwajibikaji huu unajumuisha uteuzi wa viongozi wenyc muono mzuri na ambao watawawezcsha kuyafikia malengo yao ya kimaendeleo.

Hakika, mustakabali na uwepo wa eneo la ugatuzi utakuwa zao la maamuzi ya wanaeneo.

Vilevile ufanisi wa maeneo ya ugatuzi utakuwa msingi wa ufanisi wa taifa kwa jumla.

(a) Fupisha ujumbe wa aya tatu za mwanzo kwa maneno 85-90.

(alama 8, 1 ya mtiririko)

Matayarisho:

Nakala safi:

(b) Kwa kutumia mancno 75-80, bainisha masuala ambayo mwandishi anaibua katika aya tatu za mwisho. (alama 7, 1 ya mtirin’ko)

MATUMIZI YA LUGHA: (Alama 40)

(a) (i) Eleza maana ya sauti mwambatano. (alama 2)

(ii) Andika sauti mwambatano inayotamkiwa kwenye ufizi. (alama 1)

(b) Andika sentensi ifuatayo upya ukibadilisha neno lililopigiwa mstari kuwa kielezi. Komuameshona nguo gum na kuiuza sokoni. (alama 1)

(c) Tunga sentensi mojamoja kubainisha: (alama 4)

(i) kihusishi cha wakati

(ii) kivumishi cha pekee chenye maana, “bila kubagua”.

(d) Andika sentensi ifuatayo katika hali yakinishi.

Askari wasipopiga doria wala kushirikiana na raia hawatakuwa wamctuhakikishia usalama. (alama 2)

(e) Bainisha mofimu katika neno: atamnywea (alama 3)

(f) Andika sentensi ifuatayo katika hali ya udogo: Madebe hayo yatasafirishwa pamoja na nyundo hizi. (alama 2)

(g) Ainisha vishazi katika sentensi ifuatayo: Ingawa mshahara wake si mkubwa anaikimu familia yake. (alama 2)

(h) Tunga sentensi tatu kuonycsha matumizi matatu tofauti ya kiambishi ‘li’. (alama 3)

(i) (i) Eleza maana ya sentensi ya masharti. (alama 1)

(ii) Tunga sentensi ya masharti. (alama 2)

(j) Tumia kiwakilishi cha ‘a’ unganifu katika sentensi kuonyesha

(i) umilikaji (alama 2)

(ii) nafasi katika orodha au nafasi katika kundi (alama 2)

(k) Tunga sentensi yenye kikundi tenzi chenyc muundo ufuatao

Kitenzi kisaidizi, kitenzi kikuu, nomino (alama 2)

(1) Tunga sentcnsi mbili kuonyesha matumizi mawili tofauli ya kistari kirefu. (alama 2)

(iii) Unganisha sentensi zifuatazo kuwa sentensi moja bila kurudia kitenzi.

Osore amempigia Ngungui simu. Ngungui amempigia Osore simu.

(n) Andika upya scntensi ifuatayo ukibadilisha vitenzi vilivyomo kuwa nomino: Mayaka anapotumbuiza huchekesha sana.

(0) Andika maana tatu za nenoz kanda.

(p) Andika visawe viwili vya nahau: enda kombo.

ISIMUJAMII: (Alama 10)

Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.

Haya ng‘ara Ng’ara leo! Nguo motomoto. Ng’ara leo kwa bei rahisi. Hamsini hamsini shati. Kuona ni bure. Bure kwa bure. Shika mwenyewe ujionee. Bei nafuu. Bei ya starehe. Haya haya. Usikose mwanangu! Hamsa! Fifiy! Hamsa! Fifiy! Hamsa na nyingine.

(a) Bainisha sajili ya mazungumzo haya.

(b) Eleza sifa nane za sajili hii kwa kurejelea kifungu hiki.

4.23 Kiswahili Paper 3 (102/3)

SEHEMU A : FASIHI SIMULIZI

1 Lazima

(a) Huku ukitoa mfano, eleza maana ya vitanza ndimi. (alama. 2)

(b) Fafanua majukumu sita ya vitanza ndimi katika jamii. (alama 6)

(c) Eleza mbinu sita unazoweza kutumia kalika kukusanya na kuhifadhi habari kuhusu vitanza ndimi. (alama 12)

SEHEMU B: RIWAYA

Said A. Mohamed: Utengano

Jibu swali la 2 au la 3.

2 “Walifanya kazi, walimenyeka,

Lakini walilala na njaa

Njaa, ndiyo ilikuwa misumeno

Iliyokeketa matumbo yao, …”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili. (alama 4)

(c) Kwa kurejelea riwaya, onyesha jinsi wanyonge walivyomenyeka. (alama 12)

3 Jadili uhusiano uliopo kati ya wahusika na maudhui kwa kurejelea wahusika wafuatao:

(a) Shoka (alama 10)

(b) Kazija (alama 10)

SEHEMU C: TAMTHILIA

T. Arege: Mstahiki Meya Jibu swali la 4 au Ia 5.

4 Jadili mchango wa Wanacheneo katika kuivunja jamii yao. (alama 20)

5 “Ndiyo hivyo bwana. Elimu yetu hapa ni ya kawaida mno. Haina kubwa la kumfaa mtoto mwenye mzazi anayeona mbali.“

(a) Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)

(b) Bainisha tamathali ya usemi inayojitokeza katika dondoo hili ukirejelea msemaji wa kauli hii. (alama 2)

(c) Kwa kurejclea tamthilia, fafanua mifano mingine saba ya matumizi ya tamathali uliyotaja katika (b) hapo juu. (alama 14)

SEHEMU D: USHAIRI

Jibu swali la 6 au la 7.

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana,

Nikaiga rika langu, kwa vileo na mbio za wasichana,

Kiwa ni riziki yangu, mapokeo, kuoa na kuona,

Ni wakati utanena.

Nashukuru kwa ugumba, wenye ndimi, wanipagazao nao,

Wapitao wakiimba, eti mimi, ningapenda hali zao,

Haupandiki mgomba, wana nyemi, fisadi wa hadhi zao,

Eti ni kwa raha zao.

Ni lipi lenye kukera, kwa Muumbi, marufuku kwenye misa,

Ni mtu kuwa hawara, wa vitimbi, ama alozawa tasa?

Ugumba na ukapera, sio dhambi, wala haujawa kosa,

Waama sina makosa.

Bora tungeni vitabu, magazeti, mutangaze kwa rediyo,

Muwaite watribu, kina Siti, watuzwa ilimu hiyo,

Na zaidi muhutubu, kwa umati, muwambe ambayo siyo,

Kwalo sichafuki moyo.

Hidhuru yote ni bum, sio kitu, kudhiki asodhikika,

Siwi nikaona ghere, lailatu, nyota njema itafika,

Kwa shangwe na njerejere kila mm, mdomo utafumuka,

Akiri amejibika.

(Mwalaa M. Nyanje)

(a) Eleza jambo ambalo mzungumzaji (nafsineni) katika shairi hili anasingiziwa. (alama 2)

(b) Fafanua mambo matano ambayo mzungumzaji (nafsineni) anapinga katika shairi hili. (alama 5)

(c) Eleza umuhimu wa viishio vya beti za shairi hili. (alama 2)

(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari. (alama 4)

(e) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 5)

(O Bainisha matumizi mawili ya tasfida katika shairi hili. (alama 2)

Soma shairi lifuatalo kisha ujibu aswali.

Huno wakati mufti, vijana nawausia,
Msije juta laiti, mkamba sikuwambia,
Si hayati si mamati, vijana hino dunia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

Japo aula kushufu, na machoni vyavutia,
Dunia wana dhaifu, yaugua nisikia.
Vijana nawasarifu, falau mkisikia,
Ukiona vyang’aria, tahadhari vitakula.

Jepusheni na zinaa, mlale penye sharia,
Msije andama baa, makaa kujipalia,
Jepusheni na zinaa, madhara kukadiria,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

Ngawa waone wazuri, nadhifu kukuvalia,
Wajimwaie uturi, na mapoda kumichia,
Si mlango nyumba nzuri, ngia ndani shuhudia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

Wawapi leo madume, anasa walopapia?
Wamepita ja umeme, leo yao sitoria,
Shime enyi wana shime, bora kumcha Jalia,
Uonapo vyang’aria_ tahadhari vitakula.

Nambie faida gani, nambie ipi fidia?
Upatayo hatimani, waja wakikufukia,
Ila kufa kama nyani, kasoro yako mkia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

Kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia,
Ujifanyc kama kwamba, u jiwe huna hisia,
Wakwambe watalokwamba, kwa lolote vumilia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

Vyatiririka liriri, vina vyanikubalia,
Alo bora mshairi, pa tamu humalizia,
Nahitimisha shairi, dua ninawapigia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

9. Ewe Mola mtukuka, si shaka wanisikia,
Wakingie wanarika. na anasa za dunia,
Amina wangu Rabuka, dua yangu naishia,
Uonapo vyang‘aria, tahadhari vitakula.

(Mwalaa M. Nyanje)

(a) Eleza ujumbe wa shairi hili. (alama 4)

(b) Fafanua kwa kutoa mifano, mbinu nne alizotumia mshairi kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika shairi hili. (alama 8)

(c) Nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili inasema na pande mbili. Zieleze pande hizo. (alama 2)

(d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili. (alama 3)

(e) Bainisha toni ya shairi hili. (alama 3)

SEHEMU E: HADITI-II FUPI

K Walibora na S. A. Mohamed: Damu Nyeusi na Hadirhi Nyingine

“Kikaza” (Robert Oduori)

‘Wakaacha chungu kinatokota – bila kuivisha chakula‘. Kwa hakika walijibu, “Ndio mtindo, na sisi rulifuata mitindo.”

(a) Fafanua muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Onyesha jinsi Wanatekedc wanavyofuata mitindo na kuacha chungu kinatokota bila kuivisha chakula. (alama 16)

2013 KCSE Kiswahili Past Paper-Marking Scheme/Answers

5.2.1 Kiswahili Paper 1 (102/1)

1.Huu ni utungo amilifu. Vipengele viwili vikuu vya utungo wa aina hii vishughulikiwe:

(a) Maudhui;

(b) Muundo.

Muundo wa memo Vipengele vifuatavyo vya kimsingi vizingatiwe.

(H) (i) Nembo na anwani ya Kampuni ya Jitihada. Iandikwe juu, katikati mwa karatasi wala si juu pambizoni kama ilivyo katika barua rasmi ya kawaida Anwani inaweza kujumuisha mahali, mtaa, barabara au jengo ambamo kampuni ya Jitihada inapatikana. Kwa mfanoz Mtaa wa Viwandani, Barabara ya Tungama, n.k; anwani ya bama pepe, tovuti na kipepesi (faksi).

(ii) Nambari ya marejeleo/kumbukumbu ya marejeleo. Kwa mfano: Kumb./ Rej. JIT/ JUMLA/NIDHAMU/2013/2

(iii) Tarehe – inaweza kuandikwa pambizoni kwenye mstari mmoja na nambari ya kumbukumbu.

(iv) Mtajo

(a) Kutoka Kwa: Meneja

(b) Kwa: Wafanyakazi wote

(v) Mada/Kuhusu: Ukiukaji wa maadili ya kikazi

Au

Mada: Onyo kuhusu ukiukaji wa maadili ya kikazi

(vi) Utangulizi

Mtahiniwa atangulize kiini cha memo. Kwa mfano: mtindo ufuatao unaweza

kufuatwa:

Ripoti zilizowasilishwa katika afisi hii na wakuu wa vitengo mbalimbali zimébainisha kudorora kwa maadili ya kikazi …,’n.k Hoja zipangwe ki – aya.

(viii) Hitimisho (kimuundo)

Mtahiniwa ahitimishe utungo wake.

Hapa anaweza kujumuisha hatua ambazo zitachukuliwa kwa atakayeendelca kukivi‘ maadili ya kikazi.

(ix) Kimalizio Muundo wa mwisho wa memo udhihirike kama ifuatayo:

(b) (i) sahihi

(ii) jina

(m) cheo (si lazima) kwa vile ametaja tayari.

(iv) Nakala kwa, kwa mfano,

(a) Mkurugenzi

(b) Wakuu wa vitengo

(Nakala si lazima)

Maudhui “

Mtahiniwa aibue hoja zinazohusiana na kutozingatia nidhamu kazini. Baadhi yazo ni: Kuchelewa kazini Kuondoka mapema Kuzembea kazi/kutofikia malengo Matumizi mabaya ya rasilimali za kampuni Mahusiano yasiyoruhusiwa, kwa mfano ya kimapenzi Mawasiliano yasiyofaa, kwa mfano yanayoeneza kashfa dhidi ya wafanyakazi wengine au viongozi Mavazi yasiyo na staha Kudai malipo ghushi Kutoa siri za kampuni Kuhusika katika biashara/shughuli inayoendelezwa na kampuni ya Jitihada Mapendeleo kazini, kwa mfano kuhusiana na utoaji wa nafasi za kujiendeleza Utoaji na upokeaj i wa rushwa Kutoheshimu /kutozingatia haki za wafanyakazi wenye mahitaji maalum Kushusha hadhi ya kampuni kupitia mwenendo wako Kutumia muda wa kampuni kujiendelcza masomoni bila kufidia. Matumizi mabaya ya vileo Kutoa zabuni kwa njia ya mapendeleo Kutowaheshimu wakuu wako/kudhalilisha hadhi ya wakuu Kukosa kuwajibikia makosa pale yanapotokea Kuendcleza dhuluma ya kimapenzi Kummia mali ya kampuni bila idhini kujiendeleza Hitimisho (kuhusiana na mada) Hitimisho inaweza kujumuisha hatua ya kinidhamu kulingana na sera za kampuni, k.v onyo, kusimamishwa kazi kwa muda na kufutwa. Mtahiniwa anaweza pia kuwahimiza wafanyakazi kuzingatia maadili ya kikazi (bila kutoa onyo) ili kufanikisha utendakazi na maendeleo ya kampuni. –

Tanbihi

Kwa vile hili ni onyo, mtahiniwa anahitajika kutumia lugha yenye toni kali au inayohimiza nidhamu kazini.

Mtahiniwa anaweza kufafanua kosa na hapohapo akataja hatua ya kinidhamu.

Kaida nyingine zote za usahihishaji wa karatasi hii zizingatiwe.

3. Hii ni insha ya mjadala. lfuale kanuni za mjadala ambapo patakuwa na hoja za kuunga mkono na za kupinga.

Kflmfillflllfl (i) (ii) (m) (W) (V) (vi) (vii) (vm) (ix) (X) (Xi) Hatari za kuangamia kwa lugha ambazo hazitumiki kwa wingi katika mawasiliano ya simu tamba . Kupalilia uraibu wa matumizi ya rununu, vijana kujizika katika matumizi ya rununu ‘ kiasi cha kufifilisha utendaji wao kielimu Kuchipuka na kustawi kwa aina mpya na nyeti za uhalifu kama vile utapeli Kuporomoka kwa misingi ya familia, ikiwa mume/mke atamdhibiti mwenzake kwa kutaka kusoma ujumbe wake mfupi au kuchunguza nani wanaompigia mwenzake simu, mtafaruku unaweza kuzuka. Pia jamaa nyingi huhiari kupigania simu badala ya kuonana aria kwa ana, hivyo kupujua mshikamano wa kifamilia Kuvuruga lugha/sarufi. Watu wamezoea kuandika kwa ufupi. Kudanganya katika mtihani, hivyo kupujua thamani ya mitihani. Kuzorota kwa maadili, k.v kuharibia mm sifa kupitia ‘facebook’, kudanganya moja kwa moja pale ulipo n.k. Kudhalilisha ubunifu/wizi wa kiusomi. Baadhi ya watu hutumia simu kuiba mawazo ya wengine. Wizi wa ubunifu wa kazi za kisanii ambazo hazijapewa hakimiliki Kurahisisha uporaji na unyakuzi wa malighafi za mataifa yanayoendelea kupitia kwa mtandao Upujufu wa maadili, vijana kutazama filamu chafu. flgig za kgpigga

Rununu zina manufaa chungu nzima kama vile: Kuleta wanadamu pamoja cluniani na hivyo kupunguza tuhuma zinazoelekea kuleta vurugu kwa watu kutofahamiana Usambazaji wa teknolojia inayorahisisha maisha ya wanadamu kote duniani kupitia kwa huduma zinazotolewa ria simu. Kuendeleza biashara – kubadilishana bidhaa na pesa kupitia mtandao kama vile MPESA. Hurahisisha huduma za benki. Mtu anaweza kufikia akaunti yake kupitia kwenye rununu. Huwa na vifaa kama vile vikokotoo vya kurahisisha kufanya hesabu. Ni chornbo cha burudani – vijana hupata michezo mbalimbali. Huimarisha utafiti. Mtu anaweza kufanya utafiti kupitia kwenye rununu. Huweza kutumiwa kupigia picha, hivyo kuokoa pesa ambazo zingenunulia kamera au video. Mtu anaweza kuwasiliana na familia yake kutoka mbali, hivyo kuokoa muda na fedha ambazo angetumia kusafiri. Mtu anaweza kuhifadhi msahafu(Biblia au Korani) kwenye simu, hivyo kujikuza kiroho kila mara. Ni njia ya kupata habari kutoka kwenye mashirika ya usambazaji wa habari. Baadhi ya rununu zina redio na hata runinga. Mtu anaweza kusikiliza na kutazama habari hata akiwa safarini. Hufanikisha kuwanasa matapeli na magaidi. Baadhi ya rununu huonyesha simu ilipopigiwa hivyo kusaidia kudhibiti mitandao ya uhalifu. Huduma ya simu tamba ni njia ya kujipatia riziki. Wapo raia walioanzisha biashara ya MPESA, na wengine ukarabati wa rununu zilizoharibika. Hili limepunguza makali ya uhaba wa nafasi za kazi nchini.

Tanbihi

l Mtahiniwa anaweza kujadili upande mmoja, kwa mfano, hasara tu. Huyu atahitajika kufafanua kikamilifu angaa hoja 5 ili kukadiriwa vyema kimaudhui.

2 Wapo watakaosema moja kwa moja kuwa simu tamba imeleta faida tu. Hawa pia wajadili angaa hoja 5 ili kukadiriwa vyema kimaudhui.

3 Watakaojadili pande zote mbili sharti wafafanue angaa hoja 3 kuunga na 2 kupinga/au 3 kupinga na 2 kuunga, kisha waonyeshc msimamo wao. ‘ »

4 Kuna yule atakayejadili pande zote mbile bila kuonyesha msimamo. Huyu ni mtu baki – amepungukiwa kidogo 5 Kaida nyingine zote za usahihishaji wa karatasi hii zizingatiwe.

Hii ni insha ya methali. Kisa kidhihirishe maana ifualayoz Usimpuuze mtu ambaye alikusaidia awali; au usimpuuze mtu ambaye unahitaji msaada wake ati kwa sababu amekufaa tayari na unahisi kwamba humhitaji tena. Huenda ukamhitaji mtu huyo baadaye.

Au Usivipuuze au usividharau vitu au hali ambayo ilikufaa awali. Huenda ukavihitaji baadaye.

Kisa kinaweza kudhihirisha hali zifuatazo

(i) Mhusika ambaye ameishi mahali kwa muda (labda amepewa hifadhi na ndugu au familia) kisha anapofanikiwa anawadharau.

Kisa kionyeshe hasara / tatizo linalotokana na kupuuza huku. Pengine mhusika anaweza kuhitaji msaada, japo kidogo, wa familia hii na kuona aibu kuomba. (ii) Mwajiriwa ambaye amefanya kazi katika kampuni fulani kwa muda, kisha anapopata kazi kwingine anajiuzulu kwa dharau. Wakati fulani patokee jambo linalomhitaj i kupata barua kutoka kwa wakuu wa kampuni hiyo, kisha ahasirike kwa kuona aibu kuomba.

(iii) Mwanafunzi ambaye baada ya kukamilisha masomo anatenda mambo kama vile kuwakosea walimu heshima, kuharibu mali ya shule, bila kuwazia kwamba atahitaji barua ya marejeleo kutoka kwa wakuu wa shule. n.k

(iv) Mtu ambaye anakitelekeza kifaa chake kikuukuu kwa kununua kipya. Patokee wakati ambapo hicho kipya kimeharibika na hawezi kukitumia kile cha zamani kwa vile hakukitunza.

Tanhihi

1 Kisa kinahitajika kuonyesha hali mbili: kudharau na kuathirika.

2 Wale ambao wataonyesha kudharau bila kuathirika watakuwa wamepungukiwa tu kimaudhui, hawajapotoka. Wakadiriwe ipasavyo kulingana na vigezo vya kutathminia (mwongozo wa kudumu).

3 Wale ambao wataandika kisa kisichohusiana kabisa na methali ndio ‘atakaokuwa wamepotoka kimaudhui. Hawa wawekwe katika kitengo kilichopendekezwa na vigezo vya kutathminia (mwongozo wa kudumu).

4. Watahini wawe makini zaidi. Mtahiniwa anaweza kudokeza athari kwa neno, kirai kimoja, au sentensi tu.

Athari pia inaweza kudokezwa kama lahadhari na mhusika mwingine katika hadithi, akamwambia yule anayedharau vitu an watu waliomfaa.

Maneno kiini katika swali hili ni kudunda na matarajio. Hali inayodhihirika katika mdokezo huu ni wasiwasi au taharuki.

Kisa kidhihirishe:

(a) Mhusika anayetarajia jambo.

(b) Jambo ambalo linatarajiwa – kwa mfano:

(i) kutangazwa kwa matokeo ya mtihani

(ii) matokeo ya mashindano

(iii) uchunguzi wa kiafya

(iv) kukutana na rafiki ambaye mmetengana kwa muda

(v) majibu kwa rai au swali, kwa mfanoz ombi la posa au ndoa

(vi) tangazo la kizuizi cha ndoa kwenye harusi yake kanisani au msikitini

(vii) kutawazwa kama kiongozi wa dini kama vile kasisi

(viii) kuwasili katika nchi ngeni

(ix) mwanzo wa safari kwenda nchi ngeni

(x) mwanzo wa mashindano au mbio fulani; mhusika anangojea kupulizwa kwa kipenga

(xi) siku ya kwanza katika kidato cha kwanza, mhusika anangoj ea kuingia kwenye afisi kusajiliwa

(c) Baada ya kuandika kauli hii ya mwanzo: Mtahiniwa anaweza kurudi nyuma (kutumia mbinu rejeshi), akasimulia kisa hadi akafikia hali ambayo anatarajia jambo hili.

Kwa mfano, mbinu rejeshi inaweza kuonyesha uchumba, pingamizi, kisha arusi arnbapo anahofia kuwa huenda pakatokea mtu akaipinga ndoa hii.

Anaweza pia kusimulia maisha yake shuleni, kufanya mtihani na sasa anatarajia kutangazwa kwa matokeo. Mtahiniwa anaweza kuandika kauli ya kuanzia, kisha akafululiza moja kwa moja kusimulia yaliyotokea baada ya jambo analotarajia msimulizi.

Kwa mfano: anaweza kutangazwa kuwa mwanafunzi bora zaidi; kisha asimulie kuhusu maisha yake baada ya hayo. Msimulizi anaweza kuwa aliyohofia, kwa mfano, kupingwa kwa ndoa yake yametokea, upeo wa chini au mporomoko wa maisha yake ukatokea.

Kisha asimulie masaibu yake hadi anapofikia hatua ya kujiokoa au kudidimia zaidi katika majonzi, n.k

Tanhihi

1. Mtahiniwa atakuwa gmgpgtgka kimaudhui ggjgjg kitakosa kuoana na kianzio, hivyo kuandika yasiyohusiana na swali.

2. Mtahiniwa akikosa kuanza kwa_kauli aliyopewa lakini kisa chake kioane na kiini cha swali, atakuwa hajapotoka kimaudhui, amepungukiwa kimtindo. Akadiriwe kulingana na masimulizi yake.

3. Atakayekosa kuanza kwa kauli hii, na kisa kisioane na kiini cha swali atakuwa amejitungia swali.

4. Kwa vyovyote vile lazima pawe na jambo linalotarajiwa, na ambalo linaweza kuathiri mkondo wa usimulizi, ukaelekea nyuma au mbele. Mgghini agitargijg tg mhjgg reigghi.

5. Kaida zote za usahihishaji wa karatasi hii zizingatiwe.

5.2.2 Kiswahili Paper 2 (102/2)

1. Ufahamu

(a)Kuharibika kwa miundomsingi/barabara mbovu Mishahara duni Malalamishi yao kutosikilizwa Kutothaminiwa kwa utaalamu Kukosa huduma za kimsingi k.v. maji Kuvutiwa na maisha ya kuridhisha huko ng’amb0 Kutokuwa na matumaini ya mustakabali mwcma nchini.

4×1-alama4

b) Masika ni hali nzuri au manufaa. Ng’ambo kuna maisha ya kuridhisha kama vile kuthaminiwa kwa wanataaluma.

Hata hivyo, kuna dosari zifuatazo: Upweke Ubinafsi Baridi

2 x 1

(Jumla – alama 3)

c) Umma kutofaidika kutokana na huduma za wataalamu wake licha ya kuwafadhili Kuwaachia mzigo wa kazi wataalamu wachache waliobaki Kuwapoka riziki wafanyakazi, k.v. walioajiriwa na wataalamu hawa Kulazimika kufanya kazi kwa saa nyingi, kama vile Dkt. Tabibu 3xl- alama3

d) Huwezesha kuwasiliana na jamaa walio mbali, kwa mfano, Daktari na rafiki yake wanawasiliana kwa simu. Huwezesha kuwafikia watoaji huduma patokeapo dharura, kwa mfano Daktari anapigiwa simu nyumbani. Hurahisisha usafiri – gari la Daktari. Hurahisisha kupata huduma ya karibu ya maji- bomba la maji nyumbani kwa Daktari.

3×1-alama3

e) Kuyapa mji – kuyawazia/kuyapa nafasi ya kuyajibu Fukuto – wasiwasi/mashaka/dukuduku/kutokuwa na utulivu/hamaniko

2 x 1 – alama 2

2 a)Katiba mpya iliidhinisha mfumo wa ugatuzi ambao hupunguza mamlaka ya serikali kuu kalika usimamizi wa rasilimali. Eneo la ugatuzi hutwaa kiasi fulani cha mamlaka. – Ugatuzi utahakikisha usawa wa kimaendeleo nchini kinyume na awali. Serikali isaidie maeneo yote kujiimarisha. Maeneo yaweke mikakati ya kutafiti na kubainisha rasilimali/zilizomo. Kuvumbua rasilimali mwafaka kutasaidia ustawi. Wanamaeneo watafute mbinu za kuongezea thamani rasilimali. Kilimo cha ufugaji ni nguzo ya maeneo mengi na kinahitaji kuimarishwa kwa kuandama mbinu za kisasa za uzalishaji. Ipo haja ya wanaeneo kukabiliana na matatizo yanayohusiana na soko ili kukinga dhidi ya kupoteza wateja. Ipo haja ya kujenga viwanda vya kuchinjia mifugo na kupakia nyama. Baadhi ya wafugaji huhasirika kwa kuuza mifugo wazimawazima. Wafugaji wengine hutapeliwa.

7 x l =7

Mtiririko =1

alama – 8

(b)Ujenzi wa viwanda vya kuchinjia na kupakia nyama utakinga dhidi ya kupoteza bidhaa zinazotokana na mifugo. Kujenga viwanda hivi kunasababisha ujenzi wa viwanda tegemezi. Hili litawezesha kuzalisha nafasi za kazi. Kutakuwa na kuongezea thamani utoaji wa huduma za kijamii na kiutawala. Kuzalisha nafasi za kazi kwa vijana kutasaidia kuwaadilisha vijana zaidi. Kila eneo lina vipaumbele tofauti; wakazi wabainishe kipaumbele chao. Ugatuzi unahitaji ushirikiano.l(ila mwanaeneo awajibikie maendeleo ya eneo. Wanaeneo washiriki kuteua viongozi wenye muono mzuri. Ufanisi katika maeneo ya ugamzi utachangia katika ufanisi wa taifa kwa jumla. 6 x I = 6

Mtiririko = 1

(alama = 7)

3. a)(i) Sauti mwambatano ni sauti mbili au zaidi zinazotamkwa kama sauti moja (k.v. konsonami na kiyeyusho. Kwa mfano /tw/

Au

Sauti moja ambayo ni muungano wa sauti mbili au zaidi. Kwa mfano konsonanti mbili au tatu. Kwa mfano,/nd/ mb/ ngw/

‘ 1 x 2 – (Alama 2)

Au

Sauti ambayo huundwa kwa konsonanti mbili au tam zinazotamkwa kama sauti moja, kwa mfano, /ndw/ katika ndwelemgwfkatikajangwa

mf: / nd/ – katika ufla

(ii) / nd] – katika mwago /tw/ – katika tlalika / nw/ – katika showa /zw/ – katika tula /sw/ – katika naya /ndw/ – katika ugivya

(Alama 1)

Mtahiniwa atumie kielezi cha namna kama ifuatavyo.

(b) Komu ameshona nguo vizuri na kuiuza sokoni au Komu aliuza nguo sokoni baada ya kuishona vizuri.

(Alama 2)

c) (i) Watumie kihusishi cha wakati kama vile, kisha, tangu, halafix, kabla ya, hadi, mpaka, kwa, hata, kufikia, kuanzia. Mfano: Amekuwa hapa ta_ngg asubuhi. Aliwasili halafu akaondoka.

(Alama 1)

(ii) Watumie mzizi – 0 – ote pamoja na nomino / viwakilishi katika ngeli mbalimbali. Kwa mfanoz Mwalimu alitaka kumtuma mtoto yeyote.

Nzi hula kitu chochote.

Hakuweza kula tunda Q3. n.k

(d) Askari wakipiga doria na kushirikiana na raia watakuwa wametuhakikishia usalama. (Alama 2)

e.

(f) Videbe hivyo vitasafirishwa pamoja na viiundo hivi.

au

Vijidebe hivyo vitasafirishwa pamoja na vijijundo hivi.

2 x 1 – (Alama 2)

(g) (i) lngawa mshahara wake si mkubwa – tegemezi

(ii) anaikimu familia yake – huru

2 x l (Alama 2)

(h) Matumizi ya ‘Kiambishi ‘li’

(i) Kiambishi cha wakati uliopita – Musa afltutembelea.

(ii) Kiambishi cha ngeli – Tunda filiiva

(iii) Kiambishi cha kauli tendea – Yule alikukimbil_ia au Mtoto amekafla kigoda. 3 X 1 (Alama 3)

(i) (i) Ni sentensi inayoonyesha kutegemeana kwa matendo au hali.

(Alama l)

(ii) Watumie viambishi na maneno yanayoonyesha kuwa kufanikiwa au kutofanikiwa kwa tukio au tendo moja kunategemea kufanikiwa kwa tukio au tendo lingine. kwa mfano: nge, ngali, ki, kama, iwapo n.k.

(a) Wanafunzi wangefika mapema wangempata mwalimu.

(b) Kotu angalisoma kwa bidii angalifaulu.

(c) Mvua ikinyesha mapema tutapata faida.

(d) Iwapo unataka ufanisi jibidiishe.

Tanbihi

Mtahiniwa anaweza kuandika katika hali kanushi kama ville:

(a) Mkulima asingalipanda mapema asingalipata mazao mengi.

(b) Huyu asipojihadhari ataharibikiwa.

(c) Iwapo hutaanza safari mapema utachelewa.

(d) Kama utaanza shughuli mapema hutatatizika.

(e) Lazima asome kwa bidii ili afanikiwe

(Alama 2)

(i) La Katunda linapendeza.

Au

Tindi anataka cha mwenziwe.

(ii) Atumie viwakilishi vya idadi halisi vinavyotumia a – unganifu. Kwa mfano: Wa tatu atatuzwa shaba.

Au: Mwalimu anamuita wa nne.

1 x 2 – (Alama 2)

Mifano ifuatayo au zaidi inaweza kujitokeza.

Kaini: hajawahi kupalilia mtama.

(i) Hutumiwa kutilia mkazo maelezo/kutoa maelezo zaidi/kufafanua au kuonyesha kusisitiza. Kwa mfano

Alinunua matunda — maembe, machungwa na matango.

(ii) Hutumiwa kuonyesha kubadilika kwa maoni. Kwa mfano:

Waite wale — hapana, hawa.

(iii) Kuonyesha msemaji/usemi halisi, kwa mfano Utengano ni udhaifu — duma

2 x 1 (Alama 2)

(M) Sentensi ibainishe kauli au hali ya kutendeana. Osorc na Ngungui wamepigiana simu.

Au

(n) Osore ria Ngungui wamepigania simu. 1×2 (Alama 2)

Utumbuizaji wa Mayaka una ucheshi mwingi/sana.

Au

Kutumbuiza kwa Mayaka kuna ucheshi mwingi/sana.

Au

Kutumbuiza kwa Mayaka kuna kuchekesha kwingi/sana.

I x 2 – (Alama 2)

(o)Kanda

(i) kutomasa

(ii) eneo

(iii) aina ya mfuko

(iv) mlu asiyeaminika/laghai/ayari

(v) wingi wa ukanda/mshipi

(vi) malipo kwa mganga

(vii) makasia ya kuogelea

(viii) utepe/mshipi unaotumiwa kunasia sauti/picha

(ix) mtu asiyesimika/hanithi

3 x 1 (Alarna 3)

(p)(i) enda mvange

(ii) enda upogo

(iii) enda segemnege

(iv) enda arijojo

(v) enda mrama

(vi) enda benibeni

(vii) enda shoro

(viii) enda tenge

2 x 1 (Alama 2)

Isimujamii

(b) Biashara/sokoni/kunadi au kutangaza bidhaa (Alama 2)

(i) Matumizi ya chuku – kuona ni bure, bure kwa burc, bei ya starehe

(ii) Urudiaji – ng’ara, ng’ara, haya haya

(iii) Matumizi ya misimu ya biashara kama vile: nguo motomoto hamsa, ng‘ara,

(iv) Lugha shawishi – shika mwenyewe ujionee, usikose mwanangu, bei nafuu

(v) Kauli fupifupi – kuona ni bure, bei nafuu

(vi) Lugha nyepesi – kifungu chaeleweka bila tatizo.

(vii) Kuchanganya ndimi -fify fifty/Hamsa

(viii) Matini huwa fupi. Tangazo hili ni fupi.

(ix) Kuzungumza na mteja moja kwa moja – Haya ng’ara, usikose mwanangu.

(x) Kummia mafumbo ambayo huenda yasieleweke na asiyekuwa na makini.

mf. Hamsafifty/Hamsa na nyingine – kumaanisha mia, wala si hamsini.

(xi) Kujinasibisha au kujitambulisha ria mteja. Mtangazaji anamwita mnunuzi mwzmangu ili kujcnga ukuruba baina yao, hivyo kumvutia.

(xii) Matumizi ya porojo – bure kwa bure, bei ya starehe.

8 x 1 alama 8

Tanbihi

(i) Mashani yote ya usahihishaji wa karatasi ya pili yazingatiwe.

(ii) Ni muhimu mtahini kuwa makini kufasiri ipasavyo majibu ya watahiniwa asije akawahini.

5.2.3 Kiswahili Paper 3 (102/3)

FASIHI SIMULIZI

l. (a) Maana ya Vitanza Ndimi

Vitanza ndimi ni virai/vishazi au sentensi zenye sauti zinazokaribiana au zinazofanana’ kimatamshi na ambazo hutatiza rntu kuzitamka. Aghalabu huundwa kwa vitate, vitawe, au hata kurudia maneno yalc yalc katika scntensi. Kwa mfano:

(i) Wali huliwa na mwana wa liwali.Asiyekuwa mwana wa liwali hali wali.

(ii) Wali huliwa na wanawali, wasio wanawali hawali wali.

(iii) Shirika la reli la Rwanda lililiathiri lile la reli la Kenya.

(iv) Mzee aliyevaa koti lililofika gotini alianguka akaumia goti kisha koti lake lenye kufika magotini likachanika. (alama 2)

(b) Majukumu ya Vitanza ndimi

(i) Kumzoesha mtoto/mtu kuzitamka sauti au maneno vizuri.

(ii) Ni nyenzo ya burudani. Vikao vya mashindano ya utamkaji hutumiwa kuwachangamsha wanajamii.

(iii) Msingi wa kumsaidia mtolo kujua lugha kwa undani. Huundwa kwa vitate au vitawe, hivyo mtu hujifunza vipengele hivi vya lugha.

(iv) Husaidia kuimarisha uwezo wa kimawasiliano wa anayehusika. Utamkaji wa vitanza ndimi kwa kasi humzocsha mzungumzaji kuweza kuwasilisha hoja bila kusitasita.

(v) Huendeleza utamaduni. Jinsi wanajamii wanavyoshirikishwa katika utamkaji ndivyo wanavyorithishwa utamaduni wao au dcsturi yenycwe ya kushiriki katika utamkaji.

(vi) Hujcnga stadi ya ukakamavu. Kadiri mtu anavyoshiriki katika utamkaji ndivyo anavyoimarisha ujasiri wake wa kuzungumza hadharani.

(vii) Huibua ucheshi na kudumisha uhusiano mwema. Utani unaoibuliwa katika mashindano ya utamkaji ni msingi wa kujenga uhusiano.

(viii) Hukuza ubunifu. Wanajamii huweza kubuni vitanza ndimi hapohapo, wakavitamka.

(ix) Ni kitambulisho cha jamii. Kila jamii ina vitanza ndimi vyake vinavyohusu mazingira yake.

(x) Hukuza utangamano katika jamii. Vikao vya mashindano ya utamkaji huwaleta wanajamii pamoja hivyo kujihisi kuwa kundi moja.

Tanbihi Kuonya/kushauri – baadhi hufumbata maonyo/ushauri. Kwa mfano, Mzaha mzaha huzaa usaha. (6 x 1 = 6)

c. Utazamaji wa kushiriki au kutoshiriki. Mtu anaweza kushiriki katika kikao cha utamkaji wa vitanza ndimi, hivyo kujua vinavyoendelezwa katika jamii husika. Video. Mtu anaweza kupiga picha za video watu wakitalmka/wakishindana katika. utamkaji wa vitanza ndimi ili kuja kuchanganua baadaye. Matumizi ya hojaji. Mtu anaweza kuandaa maswali katika hojaji ili kudadisi kwa mfano, kama vipo katika jamii fulani, wanaohusika katika vikao vya utamkaji na uundaji wake. Kurekodi kimaandishi (kuandika) ili kuvirithisha au hata kuvichanganua baadaye. Majadiliano ya vikundi lengwa, Mtafiti anaweza kutcua vikundi, kwa mfano, vijana,i1i kuchunguza namna wanavyoviunda na kuvitamka, na athari ya vitanza ndimi hivi kwao. Mahojiano Mtafiti anaweza kuandaa mahojiano rasmi na kundi / sampuli lengwa ili kuchunguza kwa mfano, majukumu ya vitanza ndimi katika jamii husika Matumizi ya vinasa sauti na sidii ili kunasa utamkaji wenyewe na kuchanganua sifa zake. Kutumia kumbukumbu ya mtafiti mwenyewe. Utafiti ambaye in mmoja wapo wa wanajamii katika eneo analofanyia utafiti anaweza kurithisha yale anayokumbuka baada ya kuyashuhudia. Kusoma majarida na vitabu (maktabani) vyenye habari kuhusu vitanza ndimi. (6 x 2 = 12)

Hoja zifafanuliwe ili kupata alama kamili.

Utengano: Said A. Mohamed

2. a) Ni shairi analolikumbuka (Inspekta) Fadhili katika diwani yake: Kilio cha Wanyonge.

Au: Ni maneno ya Fadhili Katika diwani yake : Kilio cha Wanyange. ~ Yumo nyumbani (sebuleni)mwa Maksuudi. Alikuwa ameitwa na Maksuudi. Ameyaona mabadiliko (fanicha) katika sebule ya Maksuudi ndipo akakumbuka haya.

(4 x l = 4)

Tanbihi

Dondoo limetolewa uk. 71 – 72 Kinaya – Wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii lakini wanalala njaa Sitiari – Njaa kufananishwa moja kwa moja na msumeno. Taswira – Picha ya watu wakimenyeka/wakiteseka. Picha ya msumemo ukikeketa matumbo. Jazanda – Msumeno ni jazanda ya njaa inaydwaumiza raia. »

(2 x 2 = 4)

c. Wakulima wanalima lakini mapato hawayapati Rejelea maneno ya Shoka (Uk. 113). Wanyonge kuandamwa na magonjwa (uk. 72). Wakulima wanapunjwa; wageni k.v Marekani ndio wanaodhibiti bei za mazao. Maimuna, Dora na wenzake danguroni kwa Mama Jeni – wanashiriki ukahaba lakini mapato yanamwendea Mama Jeni. Maimuna anatumiwa na Bili Sururu kama kivutio cha walevi. Biti Sururu anamtazama na kusema kimoyomoyo atawafaa (UK.95). Anawaambia walevi amepata kisura. Kazi kwa Biti Surum inamfanya Maimuna kudhoofika kiafya. Wazazi k.v Mama Dora anamtelckeza kwa kumuuza kwa Mama Jeni. Dora anakuwa kahaba. Dhuluma katika ndoa – Tamima kutawishwa, kupigwa – Mwanasururu na kutalikiwa na Maksuudi. Dhuluma katika malezi – Maimuna kutawishwa, Maksuudi kukinyima kitoto chake na Tamima malezi ya mama na kusababisha kifo. Wanawake kubaguliwa katika eiimu. Maimuna anasomeshewa nyumbani ilhali Mussa amesoma hadi chuo kikuu. Maimuna kutumiwa kama chombo cha kuzalisha pesa pale Rumbalola – mapato yanamwendea mwingine. Maksuudi kumpokonya Mwanasumru mali na kumfanya kuishia kuwa mwendawazimu. Wizi/unyakuzi wa mali ya umma. Maksuudi kunyakua shamba la Via – kina Haji wanaishia kuwa maskini wanaomtcgcmea. Maksuudi kuwatesa wanyonge, anauza sahihi yake; anamtaka mke wa Mzee Japu kulipa shiilingi 200 kwa sahihi yakc tu (Uk. 78). Mwanasururu anamtaka Kabi kutenda yasiyofaa na baadaye kusababisha kukzxi”-.. .. kwa mguu wake. Biti Kocho na Farashuu wanamtorosha Maimuna na kumwingiza kwenyc mtandao wa ufasiki / ukahaba.

Tanbihi

a) Farashuu anamuumbua Maimuna mbele ya mchumba wake – Kabi. Anamwita mhuni na mchafu (uk.l68) Raia wametekelezwa kwenye ujinga na umaskini. Maazimio ya baada-uhuru. kutofikiwa (uk. 72). Kazija anashirikiana kimapenzi na Mussa ambaye ana umri mbichi, kwa nia ya kumtenganisha Mussa na babake. Anaishia kumfanya kupigwa na baba yake. ’ Anawatenganisha. Farashuu – kumenyeka kazini, mwanawe Mwanasururu kudhulumiwa, mazingira duni, n.k. Maksuudi – baada ya kifungo, kupoteza asilimia kubwa ya mali yake, kupoteza hadhi, kuumbuliwa na Maimuna pale Rumbalola, ukiwa unaomwandama baada ya kusambaratika kwa familia yake, kipigo na ugonjwa, Tamima kukataa kumsamehe, nk.

(a) Mnyonge anaweza kufasiriwa kwa namna zufuatazo: Maskini Asiye na mamlaka kisiasa Anayehitaji msaada Mwenye umri mdogo kuliko mwingine Aliye katika hali fulani, kama vile ugonjwa Mwana kwa mzazi Wafanyakazi

(b) Kumenyeka kunaweza kumaanisha: Utangulizi kuteseka kudhulumiwa/kunyimwa haki kuaibika kutofikia maazimio kutengwa na familia

utangulizi

Wahusika na maudhui huchangiana kujenga kazi ya sanaa. Wahusika huteuliwa kuendeleza maudhui. Matendo yao ni msingi wa maudhui. Nayo maudhui hujumuisha matukio au hali zinazowaathiri wahusika. Tabia za wahusika huathiriwa na hali au matukio yanayowazunguka

a)Shoka Anaendeleza maudhui ya ukoloni. Anapinga hali ya wafanyakazi kuzalisha mali bila kufaidika. Anaonyesha ukosefu wa uwajibikaji katika ndoa. Anamwachia Sclume mzigo wa malezi. Anaendeleza uozo wa kijamii (usherati) kwa kuhusiana na Maimuna kimapenzi. Anaendeleza ukandamizaji wa wanawake. Anamwambia Selume hatamwacha talaka, anamwachia ulimwengu umtimbe. Anaonyesha matumizi mabaya ya vileo. Pesa zake zinaishia vilabuni. Anacndeleza maudhui ya ubinafsi. Anakula nje na kuja kugawana kidogo kilichoko na wanawe. Anaonyesha changamoto zinazohusishwa na ndoa. Ingawa anamtcsa Selume, Selume bado anaishi naye kutokana na mapenzi ya Selume kwake. Ni ishara ya ubabedume Anatarajia mkewe amheshimu licha ya kwamba hamshughulikii. Selume analalamikia utumwa wa wanawake. Anaonyesha ajizi ya wanawakc / ukosefu wa wanawake kung’amua hadhi yao. Selume anadai kuteseka lakini mumewe akikosa kurudi anakwenda kumtafuta. Anachimuza / Ni ishara ya shida zinazowakabili wafanyakazi. Wachukuzi na wakulima wanafanya kazi za sulubu na hali mazao yanawaendea wageni. Ndiye anayesababisha na kukuza ugomvi kati ya Maimuna na Kijakazi, hivyo kuonyesha jinsi wanawake wanavyong’ang‘ania kuwategemea wanaume.

(5 x 2 = 10)

b) Kazija Ni kielelezo cha ukandamizaji wa jamii ya mwanamke. Anasema mamlaka, elimu na pesa zote ni kwa mwanamume. Anaendeleza upujufu wa kimaadili kwa kushirikiana na Mussa na babake kimapenzi. Anaonyesha wanawake kama vyombo vya kusambaratisha asasi ya familia. Anamtenganisha Maksuudi na Mussa. Anamtcka maksundi kuzuru kwake hata kumwacha mkewe akiwa mja mzito. Anaendeleza dhamira ya kisasi. Anamkutanisha Mussa na babakc ili kumlipizia kisasi Farashuu. Ndiye anayewafichulia raia unafiki wa Maksuudi hivyo kuendeleza maudhui ya mapinduzi. Anachangia katika mwamko wa kijamii. Anawafanya raia kutomchagua Maksuudi na Zanga.

Tanbihi Anaendeleza maudhui ya tamaa na ubinafsi. Anahusiana na Maksuudi na Mussa ili afaidike kwa fedha zao. Anaendeleza maudhui ya unafiki. Anamwita Maksuudi Bwana ili aendelee kufaidika kwake. Ni kielelezo cha ujasiri. Kule kumkabili Maksuudi katika uwanja wa uhuru kunaonyesha ukakamavu wake. Kutatizwa kwake katika ploti kunaakisi kutojengeka (kutokamilika) kwa dhamira ya ukombozi wa mwanamke. Mwandishi anambainisha tu mara_mbili katika hadithi na baadaye kumfifilisha. i Anafichua (anaonyesha) mfumo wa ubabedume. Anamchukia mwanamume kwa kuwekwa mbele. Anachukia kujipamba ili kumfurahisha mwanamume. Anaonyesha usaliti wa viongozi k.v Zanga ambaye hatimizi ahadi alizowapa waliomchagua.,p> (5 x 2 = 10)

Si lazima mtahiniwa atangulize kwa kuonyesha uhusiano kati ya maudhui na wahusika.

La muhimu ni kujadili maudhui, hali au dhamira zinazoendelezwa na wahusika aliopewa.

Mstahiki Meya: T. Arege Badala ya Meya kushughulikia matatizo ya Wanacheneo, anasema Cheneo ni kisiwa cha kupigiwa mfano. Anajifananisha na majirani dhaifu kiuchumi na kukosa kuiendeleza Cheneo zaidi. Meya anaupujua uongozi wa Cheneo kwa kuwaacha washauri wapotoshi kuuingilia. Anamhusisha Bili katika maamuzi muhimu kama vile utoaji wa kandarasi na hali Bili si mtaalamu katika masuala haya. Meya anaifilisi Cheneo kwa kuidhinisha malipo yasiyofaa kama vile nyongeza ya mshahara wa madiwani, na malipo kwa Bili kwa kutoa ushauri ambao kwa kweli unahusu wizi wa fimbo ya Meya. – Viongozi wa kidini kama vile Mhubiri wanachangia katika kudhoofika kwa uongozi wa kisiasa kwa kutomshauri Meya vyema. Anamwombea Meya ili naye (Mhubiri) afaidike kwa sadaka anayoidhinisha Meya. Viongozi wanaufisidi uchumi kwa kutotekeleza malengo ya kimaendeleo. Meya anasema yeye anazingatia maazimio ya kimilenia ambayo kwa kweli hayashughulikii; watoto bado wanakufa kwa magonjwa yanayotokana na ukosefu wa lishe. Viongozi wanawaachia wageni kuingilia masuala ya kiuchumi. Maamuzi muhimu kama vile kugawana kwa gharama ya matibabu yanatolewa na wageni na kuwafanya raia watesekc. Meya anaifanya jamii ya Cheneo kuwa tegemezi kwa misaada. Anahofia kwamba hali ya usaii ikizorota wafadhili hawatakuja. Viongozi wanaufifilisha uchumi kwa ubadhmfu wao. Meya anatumia pesa za ufadhili kununulia mvinyo kutoka ng’ambo badala ya kuanzishia miradi. Meya anapunguza kodi ya mapato ya Baraza kwa kuidhinisha kutolipa kodi kwa madiwani. Kupuuza malalamishi ya wafanyakazi kunasababisha kutokusanywa kwa pesa, hivyo kuliteteresha pato la Baraza. Wafanyakazi kama vile Waridi wanajiuzuiu wanapoona hali ni mbaya badala ya kukabiliana nayo. Viongozi wanashindwa kuwahakikishia raia usalama wa chakula. Mama anamlisha mwanawe wali na maharagwe yaliyolala na kusababisha kifo. Anasema wanakula chakula cha mbwa. Wanataaluma wanajiepusha na siasa, hivyo kutochangia kuiboresha siasa (mfano Siki). Kumpa Meya mamlaka makubwa kunachangia kupalilia udiktela badala ya demokxasia. Kutoshughulikia afya ya kijamii kunasababisha magonjwa kama vile utapiamlo yanayotokana na ukosefu wa lishe.Waridi anashangaa vipi mama anawaletea mtoto mwenye ugonjwa wa utapiamlo; kwake hili ni jambo dogo. Badala ya raia kuimarisha viwango vya climu na huduma za afya, wanawapeleka jamaa zao ng’ambo kwa huduma hizi. Meya analalamikia eiimu duni, anampeleka mwanawe kusomea ng’ambo. Anampeleka mkewe kuzaiia ng’ambo. Kwa njia hii anaujenga uchumi wa nchi husika na kuuibia ule wa Cheneo. Meya analiibia baraza na kuufisidi uchumi wake kupitia kwa kandarasi. Pia anaidhinisha wizi wa fimbo ya Meya/ardhi. Askari wanazorotesha amani na usalama wa raia. Wanawahangaisha raia kwa bunduki na vitoa machozi. Viongozi wanasababisha kuzorota kwa hali ya usafi Cheneo kwa kutoshughulikia malalarnishi ya wafanyakazi. I-Iili linailctca Cheneo aibu na kuiumbua machoni mwa jamii ya kimataifa. Wageni wanaahirisha ziara yao. Mji umejaa uvundo unaohisika hata nyumbani mwa Meya. Watu wanawachagua viongozi licha ya kujua kuwa viongozi hao wamekosa uwajibikaji, hivyo kuzizorotesha siasa za nchi/kuuzorotesha uongozi wa kisiasa. Meya anauangamiza uongozi wake mwenyewe kwa kupuuza ushauri wa Diwani wa III na Siki. Mapuuza ya Meya yanapalilia ukosefu wa utuiivu kupitia kwa migomo ya wafanyakazi. Meya analifilisha Baraza kwa kulipagaza deni. Bili anamshawishi amwambie mwanakandarasi alishtaki Baraza alipwe fidia, naye Meya apate fungu lake. Meya na madiwani wanazorotesha uongozi kwa kutumia mbinu hasi za utawala kama vile propaganda, badala ya kuyashughulikia matatizo.

5. (a) (i) Haya ni maneno ya Meya.

Tanbihi

(ii) Anamwambia Bili.

(iii) Wamo afisini mwa Meya.

(iv) Meya anaelezea sababu za kuwapeleka wanawe ng‘ambo_kusomea huko.

Dondoo limetolewa uk.25.

Nakala nyingine zinaweza kutofautiana kiukurasa. (b)Kinaya, Meya anaikosoa elimu ambayo anastahili kuiboresha. (alama 2)

an Kejelildhihakal stihizai. Meya kuidunisha elimu. Meya anajidhalilisha kwa kudunisha elimu ambayo anastahili kuiboresha mwenyewe. (alama 2)

Kinaya

(i) Kauli ya Meya inadokeza kuwa yeye ni mzazi mwenye busara (kuona mbali) na hali anahiari kutumia pesa nyingi kuwasomeshea wanawe ng‘ambo badala ya kuboresha elimu humu.;

(ii) Meya anawadanganya raia kwamba dawa zimeagizwa ilhali sivyo, hatutarajii haya kutoka kwa kiongozi.

(iii) Meya anadai Cheneo ni kisiwani cha hazina na hali watu wanakufa (yule mtoto) kwa kukosa huduma za afya.

(iv) Badala ya Meya na madiwani kuendeleza mpango wa kimaendclco wa mji, Meya anadai kwamba wanathamjni malengo ya kimilcnia na hali kwa kweli hata haya hayashughulikiwi.

(v) Meya anamruhusu Bili kuiba fimbo ya Meya ambayo kwa kweli ndiyo kitambulisho cha umeya.

(vi) Meya anampeleka mkewe kujifungulia ng’ambo badala ya kuimarisha huduma za kiafya Cheneo.

(vii) Meya anataka mwanawe apate uiaia ng’ambo na hali yeye ni kiongozi anayetarajiwa kupalilia uzalendo.

(viii) Meya anabadhiri mali ya umma kupitia ‘entertainment vote’, huku akidai kuwa ni matunda ya jasho lake. Haya hayazarajiwi kwa kiongozi.

(ix) Meya anaidhinisha kuongeza mishahara ya madiwani ilhali Baraza lina nakisi ya fedha.

( x)Meya kulalamikia udogo wa mayai na hali watu hawana chakula.

(xi)Meya analipagaza baraza deni badala ya kulisaidia kutumia fedha vyema.

(xii)Meya analalamikia kupunjwa kwa kuletewa viyai vidogo na hali yeye anawapa wafanyakazi mishahara duni.

(xiii) Watu wanamchagua Meya wakitarajia kuimarika kwa hali zao za maisha. Meya anaishia kuwatelekeza katika njaa na magonjwa .

(xiv) Meya anaidhinisha pendekezo la Diwani H la kuundwa kwa kamati za kuhudumu na hali anafahamu kwamba baraza halimudu gharama hii.

(xv) Ni kinaya kutarajia mama muuza ndizi kulipa kodi na hali Meya anawaruhusu walionacho kama vile madiwani na kutolipa.

(xvi) Meya, badala ya kudhibiti matumizi mabaya ya mali ya umma, anajigawia vipande vinane vya ardhi na kumgawia Bili pia.

(xvii) Ni kinaya kwa Meya kutomshughulisha Diwani III katika maamuzi yanayohusu matumizi ya fedha na hali ndiye mtaalamu katika masuala haya.

(xix)Meya anaidhinisha Baraza kutoa sadaka ya shilingi laid moja kila mwezi na hali anajua lina nakisi ya fedha.

(xx)Badala ya Meya kushughulikia matatizo ya raia, anaeneza propaganda kupitia Diwani I kuhusu kujitolea kwa Baraza kutetea demokrasia.

(7 x 2= I4)

b)Mtahiniwa anaweza kuibua hoja zifuatazo kuhusiana na kejeli.

Kejeli Anwani ya tamthilia inafumbata kejeli kwa kumwita Meya mstahiki na hali hata anaidhinisha wizi wa fimbo yake. Meya anajidhalilisha kwa kulalamikia mambo madogomadogo kama vile mayai. Uongozi wa Meya unadhihakiwa kwa kushindwa hata kuiendesha zahanati. Zahanati haina hata dawa za kimsingi. _ Meya anaikejeli elimu ya humu nchini kwa kusema ni duni mno; kwa njia hii anajidhalilisha pia kwani yeye anastahili kuchangia kuiboresha . Meya anajidhalilisha mwenyewe kwa kumwachia Bili kuliendesha Baxaza na hali Bili si mtaalamu katika masuala ya uongozi. Meya anaudunisha uongozi wake kwa kuidhinisha nyongeza ya mishahara ya madiwani huku akifahamu kwamba hazina ya Baraza haimudu kughaxamia nyongeza hii. Mwandishi anamkcjeli Meya kwa kumfanya kushindwa kung’amua udanganyifii wa Bili. Mwandishi anamkejeli Meya kwa kumfanya kutumia pesa za msaada kuagizia mvinyo kutoka ng’amb0 na kuishia kurudisha pesa hizo hizo huko ng’ambo. Meya anadai kwamba kungekuwa na Phd ya uongozi angekuwa nayo na hali anaendeleza mbinu hasi za uongozi kama vile propaganda. Meya anasawiriwa kama mwenyc mawazo finyu, anayeshindwa kuona umuhimu wa mpango wa kimaendeleo wa Cheneo. ‘ , Meya anadhihaki uongozi wake kwa kuidhinisha malipo kwa kazi ambayo haijatekelezwa. Anaidhinisha kulipwa kwa Bili. Meya anajidhalilisha kwa kulipagaza Baraza deni. Anakubali mshawasha wa Bili kwamba amwambie mwanakandarasi alishtaki Baraza n.k. Meya amajidhalilisha kwa kudai kuwa ni mzazi mwenye kuona mbali na hali hata anashidwa kung’amua umuhimu wa usafi. Pia anahadaiwa na Bili kwa urahisi.

(7 x 2= 14)

Tanbihi

(i) Hoja zinazohusu kinaya zinaweza pia kujadiliwa kama kejeli au stihizai, mradi mtahiniwa amezifafanua zikaeleweka kuwa ni Kejeli.

(ii) Mifano yote, ihusiane na Meya hata kama inawarejelea wahusika wengine.

(iii) Baadhi ya watahiniwa, ambao si makini, huenda wakachukulia kuwa tamamali ya usemi iliyotumiwa ni nahau au msemo (anayeona mbali). Hawa washughulikiwe kulingana na jinsi wanvyojieleza na kutoa mifano. Hata hivyo, mifano ya semi wanayotoa lazima, ihusiane moja kwa moja na Meya.

Ushairi

6. (a) Mzungumzaji (nafsineni) asingiziwa ugumba hasa kwa kutoshiriki mapenzi nje ya ndoa.

(1 x 2 = 2)

(b) Mambo ambayo anapinga ni: Kuiga rika; hususa kushiriki ulevi pamoja na kufukuza wasichana Mzungumzaji kupakwa topc (kuaibishwa) kwa kuwa ycye ni gumba Wamsemao kudai kuwa anatamani kuwa kama wao Eti kuwa ugumba na ukapera ni kosa Kuharibu maisha kwa ujana Kusingiziwa atapenda (atatamani) hali za wamsemao Watu kueneza uvumi kuwa yeye ni gumba (5 X l = 5

(c) Umuhimu wa viishio Viishio hivi ni vifupi na hivyo vinatoa ujumbe kwa namna iliyo madhubuti Viishio hivi vinaunga ujumbe wa kila ubeti/vinasisitiza ujumbe; wa shairi Viishio vinachimuzafkuonyesha/kubainisha dhamira au mwelekeo wa mshairi kuhusu hali ya vijana kujiingiza katika mahusiano yasiyofaa. (1 x 2 = 2)

d)Mtindo ufuatao unaweza kukubalika:

Ni jambo gani ambalo linamkasirisha Mungu ambalo halikubaliki kanisani? Je, ni mtu kuwa kahaba na mwenye vioja ama mtu aliyezaliwa akiwa tasa? Kuwa gumba au kapera si kosa na wala haliwezi kuwa kosa. Kwa kweli mimi sina makosa.

(4 x 1= 4)

e) Kila ubeti una mistari minne. Mistari mitaru ya kwanza ina viapande vitatu ilhali wa nne una kipande kimoja. Vina katika kila ldpande vinabadilika kutoka ubcti mmoja hadi mwingine. Kiishio kimefupishwa. Kila mstari una mizani 20 isipokuwa kiishio chenye mizani 8. Shairi lina beti 5.

(4 x 1 = 4) Haupandiki mgomba – hana uwezo wa kujamiiana.

(2 x 1 = 2)

7. a)Shairi hili ni wasia kwa vijana; unaowaonya dhidi ya kushiriki mapenzi. Linashauxi kuwa wanaovutia machoni wanaugua na hivyo wanaweza kuwaambukjza maradhi yasiyotjbika. Zinaa hii haichagui wala kupendelea yeyote. Hata wenyc nguvu au warembo wamesalimu amri (ubeti 4). Vijana wajikaze kuhakiksiha kuwa hawaingii kwenye mtego wa kushiriki mapenzi. Wapo watakaowasema wenyc kujitunza lakini hilo lisiwafanye kutetereka.

(4 X 1= 4)

b)Tabdila – Kubadili miendclezo ya maneno pasi na kubadili idadi ya-mizani. Neno ‘nisikia‘ lingekuwa ‘nisikie’. (i) Limetumiwa hivi ili kukidhi mahitaji ya vina. ii.Inkisafi – kufupisha maneno. Inkisaxi imetumiwa kuleta ulinganifu wa mizani. Maneno yaliyofupishwa nikama vile: ‘Sikuwambia’ badala ya ‘Sikuwaambia’ ‘Jepusheni’ badala ya ‘Jiepusheni” ‘ngawa’ badala ya ‘ingawa’ ‘waone’ badala ya ‘uwaone’ ‘mkamba‘ badala ya ‘mkaamba’ ‘ngia’ badala ya ‘ingia‘ ‘walopapia’ badala ya ‘waliopapia’ ‘watalokwamba’ badala ya ‘watakalokwamba’

iii.Miundo ngeu ya kisintaksia / kuboronga sarufi. Mpangilio wa maneno katika tungo haufuati utaratibu wa kisarufi wa lugha ya Kiswahili. Baadhi ya matumizi ya mbinu hii ni: ’

(a) ‘yaugua nisikia’ badala ya ‘nisikie yaugua’

(b) ‘si mlango nyumba nzuri‘ badala ya ‘nyumba nzuri si mlango’

(c) ‘makaa kujipalia’ badala ya ‘kujipalia makaa‘,

‘madhara kukadiria’ badala ya ‘kukadiria madhara’

‘mapoda kumichia’ badala ya ‘kumichia mapoda’

iv. Mazida – ‘vyang’aria’ badala ya ‘vyang’ara’

v. Utohozi – Sitoria – histori

Mazida na utohozi zimetumiwa kuleta urari wa vina

Mbinu (4 x 2 = 8)

Kutaja – alama 1

Kufafanua, au mfano – alama 1

(c) Pande mbili ambazo mshairi anascma nazo ni: Vijana (ubeti 1 – 8) Mungu (ubeti 9)

(2 x l = 2)

(d) Umuhimu wa maswali ya balagha. Maswali ya balagha ambayo yanalenga msomaji wa kazi ya fasihi hunuiwa kumfanya kulitafakad jambo hivyo kujifunza kwalo. Humfanya msonaji kulidadisi jambo linaloibuliwa. Katika ubeti wa sita msomaji atavuta fikra kuhusu ‘faida’ ya kuingia kwenye anasa ya kumuua. Kwa kulidadisi hili ataona kuwa hamna faida na hivyo kujirudi. Hutumiwa kusuta watu au kukashifu jambo. Ubeti wa 5 unawakashifu waliopapia anasa na kuwatahadharisha wasomaji kwa kuonyesha kuwa hatima ya anasa ni kifo. Hutumiwa kusisitiza wazo au kumfanya msomaji kushawishika na mtazamo wa msanii. Kwa mfano, katika ubeti we 6, mshairi anamshawishi msomaji kwamba hakuna faida ya kuingilia anasa. Hutumiwa kuzindua. Ubeti wa 5 unamzindua msomayi kuona kuwa hata wenye nguvu huangamizwa na zinaa

(3 x 1 = 3)

d.Toni ya huzuni kusikitika i . Anasikitikia maclhara yatakayowapata wanaoingilia, zinaa kwa kauli kama vile ‘wawapi leo madume, anasa walopapia”.7(ubeti5)

Au ii.Toni ya kunasihi au kushawishi. Anawasihi vijana kuepuka zinaa. Kwa mfano anawaambia, “kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia”. (ubeti 7)

iii.Kukejeli/kudharau/stihizai/bezo.

iv.Uchungu – anaonea uchungu tabia ya vyana.

Kulaja – alama 1

Kueleza na kutoa mfano – alama 2

(1 x 3 = 3)

8.a) Mandhari ni nyumbani mwa Mzee Babu.

Wanatekede wamekusanyika kwa Mzee Babu kujadili kuhusu mabadiliko ya hali ya anga.

Bi Cherehani na Bwana Pima ambao ndio washona kikaza wamo kikaoni.

Bwana Machupa amemwomba mzee Babu kuwafafanulia kitendawili cha hali hii ya anga Mzee Babu anawaambia wanakijiji wawaulize washona kikaza. (Cherehani na Pima)

Wanapoulizwa hawatoi jibu la kuridhisha, wanasema ndio mtindo na walifuata mLindO.

(4 x l=4)

Tanbihi

Dondoo limetolewa uk. 42

b) Maneno kiini katika swali hili ni wanavyofuata mitindo na kuacha chungu kinatokota bila kuivisha

Watahiniwa wanaweza kulifasiri swali kwa nan-ma zifuatazo: Watu/viongozi kutoshughulikia hali inayowakabili Viongozi kufuata mitindo ya uongozi ya viongozi watangulizi badala ya kuiboresha Walu kufumbia macho makosa ya viongozi Viongozi kusaliti nafasi yao kwa kuendeleza uovu na uharibifu badala ya kuukosoa, nk. Viongozi na raia kuendelcza vitendo na hali hasi kama vile tamaa na ubinafsi Raia kuwawekea vikwazo viongozi na kungojea waporomoke.

Hoja zifuatazo zinaweza kujitokeza. Kobe anachangiwa manyoya na ndege kupaa angani lakini wanapofika anakula wanavyopewa bila kuwagawia waliomkweza ila waliobahatika kupata makombo. Mtajika anahujumu demokrasia kwa kupata kura kwa iijia ya udanganyifu; Mtajika hafanyi lolote kutatua shida za wanakijiji. Tunaambiwa mambo yakiwa mabaya hasemi lolote kwani ameshapata aliyotaka. Viongozi wanawasaliti washona kikaza (wapiga kura) kwa kuwadharau, kuwapuuza na kutowathamini licha ya kwamba ndio waliowachagua. Wanakijiji (raia) wanajua Mtajika amevunja masharti ya kikaza (uongozi) lakini hawamkosoi, wananyamaza, wanayafungia macho makosa ya viongozi. Mtajika anamruhusu mkewe kukishika kikaza (kuingilia uongozi) kinyume na kaida za jamii. Bi Mtajika anavunja kanuni za uhusiano mwema hata katika sherehc. Hata anatamka kuwa hakuna kiongozi mwingine kushinda yeye. Viongozi wanayaharibu mazingira badala ya kuyahifadhi. Tunaambiwa jibu la kitendawili cha mawingu bila maji limo katika kikaza. Machupa ambayc ni msemaji wa wanakijiji si wa kutegemewa. Anafaidika kwa Mtajika. Tunaambiwa kwamba yeye huenda na (huunga) upande unaomfaidi. Tunaambiwa alijua namna ya kuishi. Viongozi wamewatelekeza raia kwenye njaa na magonjwa (uk 47). Mtajika amewaaibisha wanakijiji kwa kutokilinda kikaza (uongozi). Bi Chirenga anasema kikaza kimepasuka. Mtajika na wenzake wanaipora mali ya umma; wanaifukarisha jamii kwa ubinafsi wao. Tunaambiwa kama ni nguruwe walijua kuchagua (uk 47). Raia kutokuwa na uwajibikaji wa pamoja japo wote ni washiriki katika ushonaji wa kikaza (uteuzi wa viongozi). Wanawatarajia Bi Cherehani na Bwana Pima kuelezca kitcndawili cha kutonyesha kwa mvua (uk 42). Raia kutowajibikia vitendo vyao. Wanashiriki katika ushonaji wa kikaza (uteuzi wa viongozi) bila kuwazia uzito wa tendo hili. Wanachagua viongozi ambao wanawaathiri wenyewe (uk 43- 44). Viongozi wanakwezwa uongozini na raia kisha wanawatelekeza pindi tu wanapofika kileleni (istiara ya kobe – na ndege (uk. 44). Vikaragosi wanashirikiana na viongozi kuwadhulumu wanyonge. Kobe na vibarakala wake wananyakua kila kitu na kuwaachia wachache waliobahatika masalio (uk.44). ‘ Raia wanashiriki katika uharibifu wa mazingira na kusababisha kutotegemewa kwa hali ya anga. Mvua, ama inanyesha nyingi kupindukia, au hainyeshi kabisa (uk. 40). Machupa anawaambia wanakijiji kuwa jibu la kitendawili cha wawingu bila maji ni kikaza na raia ndio wenye kupima na kushona kikaza (uk. 46). Viongozi kuendeleza uongo na udanganyifu. Mtajika angeubadilisha ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli (uk 44). Badala ya viongozi kushughulikia uhalisia wa mambo, wanaishi katika ulimwengu wa ndoto. Hata nchi inapokumbwa na changamoto, Bwana Mtajika anaota tu badala ya kukabiliana na changamoto zenyewe (uk. 44). Hata raia wanapoutaka ushauri wake, hasemi lolote; ashapala aliyopangia kupala (uk 44). Raia wanaogopa, hivyo wanayafumbia kinywa matendo hasi ya viongozi. Tunaambiwa ni wachache wanaoweza kusema ukweli, hasa unaohusu viongozi (uk. 45). Bwana Mtajika anavunja kaida za kikaza (Kaida za uongozi) na hawamkosoi. Unafiki wa baadhi ya raia unaifanya Tekede kudorora kimaendeleo. Tunaambiwa kuwa Machupa hula kuwili. wasemayo wanakijiji kumpelekea Mtajika na hapohapo anawaonyesha wanakijiji kuwa talizo limo kwenye uongozi. Yeye anajitoa lawamani badala ya kushirikiana na raia kutatua tatjzo la uharibifu wa mazingira (uk. 46). Viongozi wanawalelekeza raia waliowachagua katika njaa, umaskini na ugonjwa. (uk. 47). Bwana Mtajika anashindwa kuulinda uongozi: anashindwa kulidhibiti taifa. Cherehani anasema kwamba ldkaza kimepasuka. Wizi wa mali ya umma unawafanya wafuasi wengine wa Mtajika kutotaka kuonekana hadharani isipokuwa Machupa ambaye anajua namna ya kuishi (uk 47). Hivyo viongozi hawadiriki kutatua matatizo ya raia. Raia wanawawekea viongozi vikwazo vinavyosababisha kuanguka kwao. Cherehani anapunguza kiwango cha kikaza maksudi; kikaza kinapasuka. (uk 48)

(8 x 2 = 16)